Sultana Written Updates Wednesday May 10 2023

Becky

Posted by kiongos on 2023-05-09 20:04:47 |

Share: Facebook | Twitter | Whatsapp | Linkedin Visits: 786


Sultana Written Updates Wednesday May 10 2023

Sultana Written Updates


Wednesday May 10 2023


Fatima ameshangaa akauliza Major,unanipiga kofi mbele ya hawa vigaragosi? Major akamwambia kwanza nitakupiga,hii ni kionjo tu,naeza kuongezea ingine ile mzima mzima. Sada ndio anaenjoy kila kitu hadi akamuita Maria,njoo huku tuachie hawa wawili watwangane🤣🤣kisha Sada akaambia Major na Sada sikiza,isiwe ni ile script yenu mbovu kwa sababu nawajua nyie sana. Asiya one kusmile venye Fatima aliekwa kofi. Fatima alishikwa an aibu akatoka tu nje na Major akamfuata.


Fatima alikuja huku nje kusikia vibaya,lakini Major akamfuata,ile barua mbona ulificha? Lakini Fatima,akamwekelea Major kofi ya kwanza. Major akashangaa lakini hata kabla hajamaliza kushangaa akaongezewa ingine na akambiwa sikiza, kama ni kuondoka unataka niondoke nitaenda niende nirent room huko nja na usisahau savings zangu unazo so nazitaka. Major kuona hivyo,akamwambia sikzia Fatima,huyu Sada amejua mjanja sana na sijui anajua jua aje kama nacreate a scene pale! Major anajifanya kwa Fatima ati ile kofi ilikua tu ya kumhadaa Sada🤣🤣🤣


Tukurupuke hadi kwa Salama. JJ akiwa amekaa hapo nje,SAlama alimletea juice na akapewa kiti akae. Ua alisimama kwa mlango akachungulia akawaona wawili wamesimama hapo. Salama alianza kuongea akaambia JJ hii nyumba alinipa shangazi yako Sada na akasema hadi mambo yatulie kwanza na najua sisi kila mtu haoa mamepitia mengi ikiwemo wewe...lakini JJ alimkatiza akambia Salama sikiza,nimetoka huko ndani nije huku nje kutuliza akili na haya maneno yenu mimi sitaki. Salama akamwambia nakuelewa lakini pia nimeona niuje nijitakaze. JJ alimwambia hapa sasa itabidi unisikize,kwanza najua Babu alitoroka wakati alijua nimekuja huku na najua mambo mengi sana mnanificha na sitaki kuuliza,so achaneni tu na mimi.


Fatima na Major waliendelea kujadili na Major akaambia Fatima,Sada ashatushinda akili na sasa yafaa tumchanganye kisha tupate mwanya tuchukue kilicho chetu na hata sasa hivi,tushachanganya Sada,hajui ukweli na uongo upi na mimi niko hapa kujifanya nampenda Sultana,ndio nitege akili za JJ na Sada,unaona enye nakacheza? Fatima akaona enyewe this makes sense,lakini hana habari,huu mchezo ni yeye anachezewa,kwa sababu wakati walihugiana,Major akajisemea enyewe wewe mwanamke una taabu,utajua hujui wakati uliingilia maisha ya Sultana,niliapa mimi na wee hadi mwisho. Kumbe Fatima pia,wakiwa tu wamehugiana,akasema enyewe huyu mwanaume ni pumbavu sana. So hawa ni wawili wanajifanya wanaaminiana na hawaaminiani hata kidogo🤣🤣


Baadaye Ua alikuja akamuulzia Salama kumeendaje? Salama akamwambia  mimi kwa sasa sina lolote la kuficha. Ua akamuuliza kama ameambia JJ ako na dada? Salama akamwambia hamna,amekataa hataki kusikia hiyo story licha ya wewe kutaka nimwambia ukweli lakini amekataa kabisa hataki kujua ukweli na nishamwambia akiwa tayari kujua akuje nimwambia. Kumbe JJ alisikia akawaambia nyie wawili sikizeni,sitaki kusikia chochote kutoka kwenu🤣🤣


JJ alikuja chumbani,Sultana akamuuliza uko sawa mpenzi,nimesikia huko nje mkiongea na akina Ua na Salama. JJ alimpanga panga Sultana akamwambia hataa usijali mpenzi na kwa sasa nataka utulie ukule chakula after hapo tukule chakula tena,sawa! Sultana kakasema sawa😂😂😂


Kwa Buya nyumbani,Buya alimpigia Sarah simu akamwambia tumeona hatutahama tena,kama Fatima anataka kuja kutukuta,acha akuje sasa. Saraha akamuuliza na Dida je,ako sawa na hili? Dida akamwambia yeah,tumejadiliana na tumekubaliana hatuhami hapa. Kisha Sarah akaambia Dida,hakikisha babako yuko salama sawa? Dida akamwambia yeah,hata sai nishamsaidia kwa jambo la divorce and now you are officially talkking to a single man😂😂Dida anatetea babake kwa Sarah😂😂


Dida alimpigia Ua simu akamwambia JJ alifanya makosa sana kukutana na Major. Ua akamwambia naelewa na please pia tusaidie huko upande kwenu,akitoka tufahamishe pia tujipange na sitaki Major akuja  kama Sultana ametoka surgery. Sada alimwambia nitahakikisha huyo mtoto namlinda sana na nashukuru sana wewe na Salama mumeeka tofauti zenu kando. Ua akamuuliza tofauti gani? Sada akamwambia acha kujifanya Ua,nani hajui wewe na Salama mna historia tangu ile wakati wa kubadilisha watoto?


Maria na yeye anapigia Asiya story but mwenye anapigiwa story ako mbali sana kimawazo hadi Maria akamuuliza shida ni nini ama uanfikiria venye Fatima amekufanyia? Asiya akamwambia hata Fatima hanitishi mimi,mawazo yangu iko tu mbali na mimi hata sina nguvu ya kubishana na Fatima kwa sababu akili yangu imegorokeka kuhusu familia yangu. Maria akamuuliza familia ipi yenye hujai ongelea hata? Asiya akmwambia nimekaa tu nikafikiria kama ni kweli ni haki mimi kufanya hii kazi na kuhusu familia yangu,iko Nairobi na hakuna mwenye anajua kwenye niko kwa sababu nilichokishuhudia na macho yangu sitawai sahau. Kumbe Asiya anatoka Kanairo😂😂😂


JJ alikuja akawaita Ua na Salama wakuje wakule. Salama akashangaa haya,kumbe JJ anajua kupika hivi,then Sultana amepata bwana. Ua akamwambia mimi maswala ya ndoa ya JJ na Sultana siamini mimi ju siamini kabisa huyu JJ,wakati Major ananitongoza hungejua atakuja kunigeuka mbele. Salama akamwambia usilinganisha JJ na mnyama kama Major. Ua akamwambia mimi Major alinipenda sana na alinipea mapenzi ya kwelikweli hadi wakati yule mwanamke Fatima akakuja hapo ndio kila kitu kilibadilika. Salama alimwambia pole bi Ua na naelewa yale umepitia kwa mikono ya Major lakini usisahau JJ ni kijana tofauti na analelewa na mapenzi tofauti sana na sidhani kama atakuja kumpiga mwanamke. Kisha Ua akauliza Salama,pia wewe na Major mlikua na uhusiano,yenu iliendaje? Salama akamwambia aah,hayo tuyaache tukange yajayo😂😂


Major na yeye ako anapanga na plan lakini Fatia alimwambia sikiza Major adui wetu ni Sada na the only plan yafaa tuwe tunafanya ni kumuondoka Sada once and for all. Major akamuuliza,unamaanisha nini ukisema kumuondoa Sada? Fatima akamwambia njia ni ile ile tu kifo,lakini Major alikataa,akamwambia umesahau macho yoote ya polisi iko kwetu sai tukifanya kitu,sisi kwisha,so hiyo plan yako achana nayo kabisa.😂😂Fatima akapewa bluetick.

Watch Videos
Search
Search
Recent Updates